Psalms 80:8-13
8 aUlileta mzabibu kutoka Misri,
ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake,
mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake,
matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
11 bMatawi yake yalienea mpaka Baharini, ▼
▼ Huenda inamaanisha Bahari ya Mediterania.
machipukizi yake mpaka kwenye Mto. ▼
▼ Yaani Mto Frati.
12 eMbona umebomoa kuta zake
ili wote wapitao karibu
wazichume zabibu zake?
13 fNguruwe mwitu wanauharibu
na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
Copyright information for
SwhKC